Jumatano, 27 Agosti 2014

VIDEO: INTERVIEW YA MIKE 100.5, TIMES FM

<iframe width="560" height="315" src="//www.youtube.com/embed/YXXvFSNJDM0" frameborder="0" allowfullscreen></iframe>

RECORDING SESSION SIKU YANGU YA KUZALIWA - JOH MAKINI


Rapa wa Kanda ya Kaskazini Joh Makini amestorisha kwamba alianza kuwa inspired kufanya Hip hop baada ya kuwaskiliza wasanii kama Saleh Jabir, Mr II Sugu na wengine wakinata na beat na kuamini kuwa inawezekana hata yeye kufanya hivyo.

Mwamba anaendelea kufunguka kwa kusema kwamba ana role models wengine wengi hata Dr dree ni moja wa Role Model wake lakini Jay z ni A list wa Role models wake ambae bado hamfananishi na Rapaz wengine New York

Akizungumza katika siku yake ya kuzaliwa tar 27/08 kupitia mahojiano na kipindi cha Power Jams EA Radio, Rapa huyo anasema, “Kuwa hivi nilivyo nilijipata nafanya hivi, ni kitu ambacho hakielezeki”.

Aidha Mwamba amekazia kwamba leo itakuwa mara ya kwanza kufanya Studio Session na Producer Marco Chali katika rekodi ya siku yake ya kuzaliwa jambo ambalo litabaki kuwa kumbukumbu.

Visit: www.michaellukindo.com

DAVINA: SANDRA ALIDHANI SITAOLEWA


Miezi miwili iliyopita baada ya Star wa filamu za kibongo aliyewahi kutamba na kundi la Kaole la Jijini Dar, Halima Yahaya ‘Davina’ kufunga ndoa kimyakimya, fununu zimeibuka kwamba muigizaji huyo hakumwalika harusini swahiba wake Salama Salmini ‘Sandra’ licha ya kwamba ndie aliye muonganishia kwa bwana harusi.
Taarifa hizi zinaonyesha kuwepo kwa dalili za uhalisia wa tukio hilo kutokana na tetesi kwamba wawili hao (Davina na Sandra) walijaribu kila mmoja kwa wakati wake kumshawishi mwanaume huyo ambae jina lake halikuwekwa wazi na mwishowe bahati kuangukia kwa Davina
Kabla ya fununu za mchapo huu kuibuka Davina aliwahi kukaririwa akisema, Siku moja tulitoka na mchumba wangu (sasa mumewe) pamoja na Sandra ili kupata chakula cha jioni, Sandra akawa anataka kuongea pembeni na mchumba wangu jambo ambalo sikulipenda hata chembe, nikamkataza ndiyo akakasirika,”.


HATA SASA KAJALA KWA PETY MAN HUTII NENO


Fununu za kuwepo kwa dalili za usaliti unaofanywa na Kajala dhidi ya mumewe ambae bado anatumikia kifungo gerezani, zimejionyesha wazi siku chache baada ya Star huyo wa ‘Bongo Muvi’ kufanikiwa kumaliza tofauti yake na aliyekuwa Miss Tanzania 2006, Wema Isac Sepetu.

Hali hiyo imejitokeza katika mazingira ambayo Kajala ameonekana kurudi Endless Fame kwa mbwembwe na makonfidensi yote ikiwa ni hatua ya kumaanisha kuwa ‘yaliopita si ndwele’ hali ambayo imezaa uhusiano wa karibu kuliko kawaida baina yake na tajiri Mtoto, Petty Man.

Hata hivyo nyota huyo (Kajala) ambae amekuwa akionekana kuspendi mshiko mrefu na maraha mengi viwanja vya kijanja kufananisha na kipato anachoingiza kwenye shughuli za sanaa, alikana kabisa kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Petty Man, wakati akijibu swali la ripota wetu kama wamerudi tena kushea shuka.

Petty Man ambae ni swahiba wa mmliki wa kampuni ya Endless Fame, Wema Sepetu kwenye raha na dhiki, alipovutiwa waya kujieleza nae alikiri kuwa na ‘Upendo wa Agape’ dhidi ya Kajala, akidai kwamba ukaribu wake na Star huyo wa Bongo Muvi ni wa siku nyingi na kwamba urafiki wao umekomaa kiasi ambacho anaweza kuthubutu kumweleza hata siri zake ili kupata ushauri wenye manufaa.


JINI KABULA AJISIFIA KUVAA NUSU UTUPU


Nyota wa zamani wa tamthilia ya Jumba la dhahabu, Miriam Jolwa maarufu kama Jini kabula ameapa kutoacha kabisa tabia ya kuvaa ‘vichupi’ akionyesha msisitizo kwamba hiyo ndio aina ya maisha aliyochagua kwasababu inamfanya awe huru.

Akistorisha na paparazi wa michaellukindo.blogspot.com msanii huyo aliendelea kusema kwamba vichupi ndio mavazi aliyokuwa akivaa tangu enzi za Utoto wake na kwamba hakuna mtu yoyote atakaye badili maamuzi yake kuhusu kubadili mfumo wake wa uvaaji.

Kabula ambae hapo awali aliwahi kujiingiza kwenye sanaa ya Muziki akiwa katika kundi la ‘Scorpion Girls’ pamoja na wasanii wengine wakike kama Rashida Wanjara na Isabela ‘Bella’, aliweka aibu pembeni na kusema, “Binadamu wameumbwa wanasema kwahiyo waache waseme alafu wakiona wametosheka watapiga kimyaa vichupi siachi”.



MKE WA MTU MTAMU - TIMBULO


Wakati vyombo vya habari vikikemea tabia zinazochochea vitendo vya ngono nje ya ndoa ili kuepuka UKIMWI, msanii wa kizazi kipya maarufu Timbulo, ameonyesha udhaifu wake kwa kiasi kikubwa kueleza namna ambavyo amekua akichepuka na mke wa mtu.

Timbulo alikiri kufanya vitendo hivyo vichafu na mke wa mtu akidai kuwa aliweza kulala na kishtobe huyo wakati wowote alipojiskia na kwamba hakuwahi kuwa na hofu juu suala la fumanizi.

“Ni kweli nilikuwa natoka na mwanadada ambaye ni mke wa mtu, ila nilikuwa sifahamu chochote kwasababu muda wowote nikimuhitaji nilimpata”,Alisema

Msanii huyo anajisahau zaidi na kumueleza ripota wa michaellukindo.blogspot.com kwamba ilifika wakati mwenye mke aligundua na kumuonya juu ya tabia yake ya uzinzi, hatua iliyompa woga hadi kufikia kuacha vitendo hivyo vya ngono zembe.


THEA AITOSA BONGO MUVI



Siku chache baada ya Msanii mkubwa katika anga la filamu Bongo, Ndumbangwe Misayo, ‘Thea’ kubadilishwa Jina na mumewe Michael Sangu ‘Mike’ na kuitwa Salome Urasa Sangu, muigizaji huyo juzi kati alimwagia paparazi wetu mastori kuhusu mpango ya ujio wake mpya baada ya kuwa kimya kwa kipindi kirefu.

Salome Sangu ‘Thea’ katika hali ya uchangamfu na kujiamini alikanusha mbele ya ripota wa umbea huu kuhusu fununu za kuitosa Bongo Muvi akidai kwamba kimya chake kilitokana na kugundua kuwa ni sawa na upuuzi kuonekana kila siku kwenye makava ya filamu za kibongo wakati hana pesa mfukoni.


Akiendelea kuzungumza kwa makonfidensi yote kuhusu mkakati madhubuti alioandaa dhidi ya kazi zake mpya za filamu Star huyo anasema , “Wapenzi wa Filamu za Bongo watarajie kazi nzuri kutoka kwenye kampuni yetu mimi na mume wangu,muda wowote kutoka sasa zitaanza kuingia sokoni”.