Jumatano, 27 Agosti 2014

JINI KABULA AJISIFIA KUVAA NUSU UTUPU


Nyota wa zamani wa tamthilia ya Jumba la dhahabu, Miriam Jolwa maarufu kama Jini kabula ameapa kutoacha kabisa tabia ya kuvaa ‘vichupi’ akionyesha msisitizo kwamba hiyo ndio aina ya maisha aliyochagua kwasababu inamfanya awe huru.

Akistorisha na paparazi wa michaellukindo.blogspot.com msanii huyo aliendelea kusema kwamba vichupi ndio mavazi aliyokuwa akivaa tangu enzi za Utoto wake na kwamba hakuna mtu yoyote atakaye badili maamuzi yake kuhusu kubadili mfumo wake wa uvaaji.

Kabula ambae hapo awali aliwahi kujiingiza kwenye sanaa ya Muziki akiwa katika kundi la ‘Scorpion Girls’ pamoja na wasanii wengine wakike kama Rashida Wanjara na Isabela ‘Bella’, aliweka aibu pembeni na kusema, “Binadamu wameumbwa wanasema kwahiyo waache waseme alafu wakiona wametosheka watapiga kimyaa vichupi siachi”.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni