Jumatatu, 25 Agosti 2014

EXCLUSIVE: KUMBE BINTI KIZIWI ALIZAA NA MUHOLANZI, SOMA ZAIDI UFAHAMU MENGI


ALIKUA AKIJIUZA VISIWANI ZANZIBAR, ALIZAA NA MUHOLANZI

·         Alimuhonga mihela kibao ili aache umalaya lakini wapi
·         Mzungu ajuta kumjua/astaajabu licha ya ujauzito bado binti atinga viwanja usiku wa manane na tumbo lake
·         Tamaa zamponza kama fisi mzungu am'bwaga akacha


Hatimae siri imefichuka kuhusu historia ya maisha ya Sabra Khan maarufu ‘binti kiziwi’msichana aliyewahi kujipatia umaarufu mkubwa mara baada ya kushirikishwa kama Video Qeen kwenye nyimbo ya msanii wa kizazi kipya Z-Anto

Chaumbea mmoja aliebobea alivujisha kwa raha zake siri za binti kiziwi akidai kwamba kabla ya shostito huyo kujizolea umaarufu mkubwa nchini kwa kusafiria nyota ya Z-Anto, aliwahi kuishi Visiwani Zanzibar ambako inasemekana alikuwa akijihusisha na shughuli za ukahaba.

Mpashaji huyo alikamia kusimulia akikazia kuwa katika harakati za Binti kiziwi kujirusha sana viwanja vya starehe akiuza uroda, alianza kuwa bwege wa ngono zembe na mwishoe kugeuka teja wa ngono kwenye ngozi ya mteja anaedaiwa kuwa ni mzungu, raia wa Uholanzi ambapo mwishoe alinasa ki zaigoti aka ujauzito

"Mtoto wa kike kiguu na njia tumbo limekua kubwa, mzungu anahudumia kwa mbwembwe na kiingereza chote lakini mwanamke kama zoba vile yani usiku anatoroka unamkuta viwanja anakula vichwa", Alisema mpashaji huyo.

Kama ambavyo waswahili husema 'kunguru hafugiki' unaambiwa mtoto alipozaliwa baada ya mtasha kuona kicheche hasomeki aliamua bora amchukue mwanae na kutokomoea nae kimya kimya nyumbani kwao uholanzi.

Endapo utakua ni mfuatiliaji mzuri mapema mwaka huu mlimbwende Sabra Khan aka Binti kiziwi aliandikwa na kutajwa mara nyingi sana kwenye vyombo vya habari akihusishwa na tuhuma za kunaswa na dawa za kulevya huko China.

Wajuzi wa mambo wanaeleza kwamba huenda shostito huyo mwenye uraia wa Tanzania akawa alinyongwa kutokana na sheria za Jamuhuri ya china hasa unaponyakwa ukijihusisha na biashara haramu.

Rafiki wa karibu kabisa na binti kiziwi ambaye yupo hapa nchini alimfungukia mwandishi wetu akimlaani bibie Jackline Patrick aka sikio la kufa akidai kuwa yeye ndiye alimbebesha binti kiziwi mzigo huo wa madawa na kumtelekeza baada ya kubainika na kutiwa kwenye nguvu ya dola.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni