Jumatano, 27 Agosti 2014

MKE WA MTU MTAMU - TIMBULO


Wakati vyombo vya habari vikikemea tabia zinazochochea vitendo vya ngono nje ya ndoa ili kuepuka UKIMWI, msanii wa kizazi kipya maarufu Timbulo, ameonyesha udhaifu wake kwa kiasi kikubwa kueleza namna ambavyo amekua akichepuka na mke wa mtu.

Timbulo alikiri kufanya vitendo hivyo vichafu na mke wa mtu akidai kuwa aliweza kulala na kishtobe huyo wakati wowote alipojiskia na kwamba hakuwahi kuwa na hofu juu suala la fumanizi.

“Ni kweli nilikuwa natoka na mwanadada ambaye ni mke wa mtu, ila nilikuwa sifahamu chochote kwasababu muda wowote nikimuhitaji nilimpata”,Alisema

Msanii huyo anajisahau zaidi na kumueleza ripota wa michaellukindo.blogspot.com kwamba ilifika wakati mwenye mke aligundua na kumuonya juu ya tabia yake ya uzinzi, hatua iliyompa woga hadi kufikia kuacha vitendo hivyo vya ngono zembe.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni