Jumapili, 24 Agosti 2014

POMBE, WANAWAKE VYAMPONZA TUNDA MAN KUACHA SOKA


Mbongofleva wa kundi la Tip Top Connection Khalid Ramadhan Tunda maarufu ‘Tunda Man’, amesema aliacha Soka na kuchagua muziki kwasababu ya masharti magumu wanayopewa wachezaji kama vile kutokunywa pombe na kuwa mbali na wanawake hususani wakati wachezaji wakijiandaa kwenda ligi kambini.

Tunda Man ambae aliwahi kucheza mpira wa miguu kwenye ligi daraja la pili 2004 kwenda 2005, chini ya kocha m’malawi, Jackson mwangama; Aliwezeshwa na Mkuu wa shule ya Sekondari Makongo Bw. Kipingu, kuingia kwenye timu ya Soka ya Yanga baada ya kugundua uwezo mkubwa aliokuwa nao.


“2004 Peter Manyika ndio alikuwa anatoka anaenda uarabuni, kwa hiyo timu ilibakia na kipa wawili tu, Mengi Matunda na Hussein Kabwe, Sasa kwasababu huwezi kucheza ligi wakati una makipa wawili ndio hapo mimi nikachukuliwa nikapelekwa kule tukawa makipa watatu”, Alisema Tunda Man

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni