Jumatatu, 25 Agosti 2014

FUPI TAMU JAMANI NDEFU INABOA - KHADIJA KOPA


Malkia wa Mipasho nchini, Khadija Omar Kopa ‘Top in Town’ amesema kwamba toleo jipya la Albamu yake kutakua na mabadiliko mengi ya kiufundi kama vile kupungua kwa urefu wa nyimbo zake kutoka dakika ishirini hadi tisa kila wimbo.

Mkali huyo alietamba na kibao cha Mjini Chuo Kikuu amesema lengo si kupunguza raha ya kucheza au kusikiliza muziki wa taarabu isipokuwa kuongeza hamu ya kusikiliza nyimbo nyingi kwa muda mfupi, akifafanua kwamba wimbo unapokuwa mrefu sana msikilizaji nae anaweza aidha kuchoka kabla wimbo haujamalizika.

Albamu mpya ikitoka kutakuwa na mabadiliko mengi na kubwa ni kipimo cha urefu wa nyimbo zote, watu wataweza kusikiliza hata nyimbo tatu kwa muda mfupi. Dakika zitapungua kutoka ishirini kwa wimbo mmoja hadi dakika tisa”, Alisema Khadija Khopa.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni