Jumapili, 24 Agosti 2014

PENZI LA JENNIFER LOPEZ LAMTESA MWANAMITINDO MARTIN KADINDA


Mwanamitindo wa Tanzania Martin Andrew Kadinda, amewataka watanzania kufahamu kwamba anamzimia kimapenzi Mwanamitindo maarufu, muigizaji mkubwa wa sinema duniani Mwanamuziki nyota Marekani, anayemiliki utajiri wa zaidi ya dola za Kimarekani 300 Milioni, Jennifer Lynn Lopez.

Akizungumza na michaellukindo.blogspot.com Martin Kadinda (27) ambae pia ni Meneja wa aliyekuwa Miss Tanzania 2006 Wema Isac Sepetu, alidai kwamba hajawahi kuona mwanamke mzuri katika maisha yake kama J-Lo, na kwamba anampango wa kufanya jina lake kuwa kubwa upesi ili aweze kukutana na Star huyo.


Mwanamitindo huyo aliongeza msisitizo kwasema, “Mimi naamini kila kitu ni bahati, kama nimeweza kufanya kazi na madizaina wakubwa naamini hata hili la kutoka na Jennifer Lopez ni dogo tu kwangu”.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni