Jumatano, 27 Agosti 2014

RAINFRED MASAKO ADAI KUWA NA GARI NI UFAHARI


Mtangazaji maarufu wa kituo cha Televisheni cha ITV Jijini Dar es salaam Tanzania Bw. Rainfred Masako, hivi karibuni ametoa mpya ya mwaka kwa kumfungukia mwandishi wa michaellukindo.blogspot.com kwamba mtu kuwa na gari ni ufahari.

Masako ambae makazi yake ni maeneo ya Mbagala, amekuwa akimaliza soli ya kiatu kwa miaka mingi licha ya umaarufu na uzoefu wake mkubwa utokanao na staili yake ya utangazaji, alidai kuwa alishawahi kumiliki gari lakini hakuona tena haja ya kuendelea kuwa na gari hilo baada ya kupata usumbufu mkubwa.

Akizungumza kwa njia ya simu Masako alisema, “Niliwahi kupata mkopo wa SACCOS ofisini kwetu nikanunua gari kwa mtu ilikuwa mwaka 1997, lakini baadae ile gari ikaanza kunisumbua kwa hitilafu za mara kwa mara za kiufundi kwahiyo mwaka 2001 ikabidi niuze”, Alisema.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni