Jumatano, 27 Agosti 2014

RECORDING SESSION SIKU YANGU YA KUZALIWA - JOH MAKINI


Rapa wa Kanda ya Kaskazini Joh Makini amestorisha kwamba alianza kuwa inspired kufanya Hip hop baada ya kuwaskiliza wasanii kama Saleh Jabir, Mr II Sugu na wengine wakinata na beat na kuamini kuwa inawezekana hata yeye kufanya hivyo.

Mwamba anaendelea kufunguka kwa kusema kwamba ana role models wengine wengi hata Dr dree ni moja wa Role Model wake lakini Jay z ni A list wa Role models wake ambae bado hamfananishi na Rapaz wengine New York

Akizungumza katika siku yake ya kuzaliwa tar 27/08 kupitia mahojiano na kipindi cha Power Jams EA Radio, Rapa huyo anasema, “Kuwa hivi nilivyo nilijipata nafanya hivi, ni kitu ambacho hakielezeki”.

Aidha Mwamba amekazia kwamba leo itakuwa mara ya kwanza kufanya Studio Session na Producer Marco Chali katika rekodi ya siku yake ya kuzaliwa jambo ambalo litabaki kuwa kumbukumbu.

Visit: www.michaellukindo.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni