Jumatano, 27 Agosti 2014

CHRISTIAN BELLA AZAMIA LEBA, JICHO LAMTOKA KAMA NGUMI


Mtunzi bora wa Mwaka wa Bendi, Raisi wa Malaika Bendi Christian Bella, amesema aliandika mashairi ya wimbo wake mpya uliotoka hivi karibuni uitwao ‘Nani kama Mama’,  kuelezea hisia zake za dhati juu ya umuhimu wa kuheshimu na kuthamini  Mama zetu, baada ya kushudia tabu aliyoipata mke wake wakati akijifungua Mtoto Hospitalini.

Christian Bella ambae amewahi kupata tuzo ya heshima kutoka kampuni ya First Entertainment inayofanya kazi zake chini ya Mkurugenzi Pauline Daniel, aliyasema hayo siku chache baada ya kujaaliwa kupata Mtoto wa Pili na mkewe (Jina tunalo).


Nilipata nafasi kuwepo wakati mke wangu akijifungua Mtoto Leba, nikawa nashuhudia kila kitu kinachoendelea, yani jicho lilinitoka siwezi kusahau nilikaa pembeni nikaangalia kwa uchungu, iliniuma sana na hapo nikazidi kupata nini maana ya thamani ya Mama”, Alisema Christian Bella.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni