Jumatano, 27 Agosti 2014

DAVINA: SANDRA ALIDHANI SITAOLEWA


Miezi miwili iliyopita baada ya Star wa filamu za kibongo aliyewahi kutamba na kundi la Kaole la Jijini Dar, Halima Yahaya ‘Davina’ kufunga ndoa kimyakimya, fununu zimeibuka kwamba muigizaji huyo hakumwalika harusini swahiba wake Salama Salmini ‘Sandra’ licha ya kwamba ndie aliye muonganishia kwa bwana harusi.
Taarifa hizi zinaonyesha kuwepo kwa dalili za uhalisia wa tukio hilo kutokana na tetesi kwamba wawili hao (Davina na Sandra) walijaribu kila mmoja kwa wakati wake kumshawishi mwanaume huyo ambae jina lake halikuwekwa wazi na mwishowe bahati kuangukia kwa Davina
Kabla ya fununu za mchapo huu kuibuka Davina aliwahi kukaririwa akisema, Siku moja tulitoka na mchumba wangu (sasa mumewe) pamoja na Sandra ili kupata chakula cha jioni, Sandra akawa anataka kuongea pembeni na mchumba wangu jambo ambalo sikulipenda hata chembe, nikamkataza ndiyo akakasirika,”.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni